17/01/2026
NINI KINAJIRI BAADA YA NDOA KUVUNJIKA KWA TALAKA?
Leo nataka niongelee mojawapo ya vitu vinavyozua mvurugano katika familia na jamii nyingi hapa kwetu Tanzania. Hapa nazungumzia mipango yote na vyote vitakavyojiri baada ya mahak**a kutoa tamko la kuivunja ndoa kwa kutoa hati ya talaka. Kimsingi, ni mambo mawili yanayojumuishwa tunapozungumzia mipango baada ya tamko la kuivuja ndoa, mambo haya ni mgawanyo wa mali na kupata haki ya kubaki na watoto.
Suala gumu linalojumuisha mgawanyo wa mali. Na kifungu cha 14 cha Sheria ya Ndoa ya 1971 kilileta mgongano mkubwa wa kitafsiri ambao ulidumu kwa miaka 10 katika Mahak**a Kuu ya Tanzania. Neno juhudi za pamoja, ndilo hasa lililoleta utata wa tafsiri kwani swali lililojitokeza ni je, kazi anazofanya mama wa nyumbani k**a kupika, kuosha vyombo na kumfulia nguo mumewe, nazo ni sehemu za juhudi za pamoja? Upande mmoja wa majaji walikubaliana na mtazamo kwamba kazi hizi nazo zinajumuishwa k**a juhudi za pamoja na upande wa pili ukikataa mtazamo huo.
Baada ya miaka 10 ya mvutano huu, Mahak**a ya Rufaa ya Tanzania kupitia moja ya shauri maarufu zaidi katika masuala ya ndo la Hawa Mohammed dhidi ya Ally Seif (1983),TLR, 32, ilitoa msimamo kwamba majukumu ya mama nyumbani nayo yanajumuishwa k**a sehemu ya neno juhudi za pamoja, kwani hata mume anahitaji chakula kilichopikwa vizuri, nguo safi na kadhalika.
Na hivi mara nyingi vinafanywa na kina mama (hasa wale wasiofanya kazi maofisini). Hata hivyo, Mahak**a ya Rufaa iliongeza kitu cha ziada kwamba, pale mwanandoa anapotenda kosa linaloathiri ndoa yake, kosa hilo linapunguza kabisa mchango wake katika juhudi za pamoja na anaweza kuondoka mikono mitupu kabisa.
Hata hivyo, wakati wa kugawanya mali za wanandoa, vitu vya kuzingatia ni maendeleo ya watoto na mila na desturi za kabila husika, inapotokea wanandoa wanatoka makabila tofauti na hivyo mila na desturi zao zinatofautiana, basi mahak**a itazingatia zaidi sheria za nchi kuliko mila na desturi za makabila hayo.
Katika shauri la Mohammed Abdalah dhidi ya Halima Msangwe (1988), TLR, 197 mahak**a iliamua kwamba mgawanyo wa mali si suala la kulipana fidia bali ni kitendo cha kumpa mtu stahiki yake kwa juhudi za pamoja za kujenga familia yao. Shauri jingine linaloleta tafsiri pana zaidi juu ya mgawanyo wa mali ni la Bibie Maulidi dhidi ya Mohammed Ibrahim (1989),TLR, 162 ambapo mahak**a ilikataa utetezi kwamba mali ya wanandoa walioachana inatakiwa igawanywe nusu kwa nusu.
Na kutoa maamuzi kwamba sheria haijatamka kwamba mali zigawanywe nusu kwa nusu, na kwamba kinachoangaliwa zaidi ni ustawi wa watoto, madeni yanayoikabili familia, labda mikopo ya benki na kadhalika, pia mila na desturi za wahusika.
Kwa hiyo kimsingi, mahak**a inatuambia kwamba hakuna fomula moja, bali maamuzi yatategemea kesi yenyewe ilivyo.
Suala la pili la msingi ni haki ya kukaa na watoto. Hili pia ni suala linaloleta migogoro na migongano ya mara kwa mara kwa watu waliotalikiana. Kitu ambacho ndugu msomaji unatakiwa kuzingatia hapa ni kwamba watoto wanaozungumziwa hapa ni wale walio chini ya miaka saba, kwani chini ya sheria hii, kuna makundi mawili ya watoto, wale walio chini ya miaka saba na wale walio juu ya miaka saba.
Kwa watoto walio chini ya miaka saba, basi kwa ujumla ni kwamba mama ndiye atakayepewa jukumu la kukaa na watoto.
Hata hivyo wakati mwingine hii haitakubalika ikiwa tu tabia na hali ya kiakili na kifedha ya mama itathibitika si shwari. Kanuni kuu inayozingatiwa na mahak**a wakati wote wa kutoa haki ya kuishi na watoto ni ustawi na maendeleo ya mtoto/watoto kwanza na si majigambo au vita ya wazazi.
Hii ina maana kwamba, ustawi wa mtoto ndiyo kitu cha kwanza na kwamba mtoto ni mali ya Jamhuri na hivyo Jamhuri ina jukumu la kuhakikisha kwamba ustawi wa mtoto unazingatiwa kwanza. Kwa mujibu wa kifungu cha 125 cha Sheria ya Ndoa, 1971, sheria imeweka wazi juu ya ni nani anaweza kupewa haki ya kukaa na watoto baada ya wazazi kuachana.
Hapa sheria inasema kwamba ni mtu yeyote anaweza kupewa haki ya kukaa na watoto ikiwa tu mahak**a itaridhika kwamba baba na mama wa watoto hao hawawezi kufanya hivyo.
Mahak**a ina uwezo wa kuamuru wapi mtoto akasome, wapi akaishi na hata wakati mwingine dini gani afuate kwa kuzingatia mazingira ya kesi yenyewe. Inapotokea mzazi mmoja akafariki, ndugu wa mzazi huyo wataruhusiwa kila wakati utakaofaa kufanya hivyo. Hata hivyo, chini ya kifungu cha 126(e) cha sheria hii, sheria imekataza kwa hifadhi ya mtoto kupelekwa nje ya nchi na mtu aliyechaguliwa kuwalea.
Katika shauri la Mariam Tumbo dhidi ya Harod Tumbo (1983), TLR, 293, mahak**a iliamua kwamba linapokuja suala la kuishi na watoto baada ya tamko la talaka, inapotokea mtoto mwenyewe akatoa maoni yake juu ya wapi anapenda kwenda kukaa ( yaani kwa baba au kwa mama), mahak**a inatakiwa kuzingatia maoni hayo ya mtoto.
Wakati hali ya kitabia, kifedha, kiakili na kimaadili inapobadilika kwa mtu aliyepewa haki ya kulea watoto, kwa mfano, mtu aliyepewa watoto hao alikuwa si mlevi kupindukia, na alikuwa ana uwezo wa kuwapeleka shule vizuri, lakini baada ya kupewa watoto anaanza kubadilika na kuwa mlevi kupindukia, au mwenye matatizo ya akili, basi upande wa pili una haki ya kwenda katika mahak**a ileile iliyompa haki ya kukaa na watoto mara ya kwanza na kuiomba ibatilishe tamko hili kwa sababu hali ya mlezi imebadilika.
Hii ni kwa mujibu wa maamuzi ya mahak**a katika shauri la Halima Kalima dhidi ya Jayantulahu (1987)TLR,147. Kwa kuhitimisha tu, mambo makuu mawili ndiyo yanayoangaliwa pale watu waliopata hati ya talaka mahak**ani wanapoanza kuangalia mipangilio baada ya talaka. Mambo haya ni pamoja na mgawanyo wa mali zilizopatikana wakati wa ndoa na pili ni suala la malezi ya watoto baada ya tamko la mahak**a la kuivunja ndoa hiyo kwa kutoa Talaka.
Lusako Mwang'onda
(Mchambuzi wa maswala ya Sheria)