02/06/2026
CLAUDIA DHAHABU ASHANGAZWA NA HASIRA DHIDI YA BARAKA CHULA: "MBONA HAMZUNGUMZII ALIYEMKIMBILIA RAIS?"
Claudia Dhahabu Kenga ameibua mjadala mtandaoni baada ya kuhoji kile anachokiona k**a viwango tofauti vya hukumu dhidi ya matukio yaliyotokea wakati wa sherehe za Madaraka Day.
Kupitia ujumbe wake, Claudia alishangaa kuona watu wengi wakikerwa na kitendo cha Baraka Chula huku akidai kuwa hakuna mjadala mkubwa unaoendelea kuhusu mtu aliyemkimbilia Rais wakati akitoa hotuba huko Ganze.
"So everyone is disappointed na Chula but sio yule alikimbilia Rais? Weuh nijeri yo story..." aliandika Claudia.
Kauli hiyo imezua hisia mseto kwenye mitandao ya kijamii, ambapo baadhi ya watu wameunga mkono mtazamo wake wakisema matukio yote yanapaswa kutazamwa kwa uzito sawa, huku wengine wakisisitiza kuwa kila tukio lina mazingira yake na linapaswa kuhukumiwa kivyake.
Je, unakubaliana na Claudia Dhahabu kwamba baadhi ya matukio yanapewa uzito mkubwa kuliko mengine, au unaamini mjadala kuhusu Baraka Chula unastahili kutokana na mazingira ya tukio lake?